Machapisho

Nimekombolewa na Yesu

1.Nimekombolewa na Yesu Aliyenirehemia; Kwa bei ya mauti yake Nimekuwa mtoto wake. Kombolewa! Nakombolewa na damu; Kombolewa! Mimi mwana wake kweli. 2.Kukombolewa nafurahi, Kupita lugha kutamka; Kulionyesha pendo lake, Nimekuwa mtoto wake. 3.Nitamwona uzuri wake, Mfalme wangu wa ajabu; Na sasa najifurahisha, Katika neema yake. 4.Najua taji imewekwa Mbinguni tayari kwangu; Muda kitambo atakuja, Ili alipo, niwepo.

Tenzi za Rohoni: Bwana u sehemu yangu

Bwana U sehemu yangu  Rafiki yangu, wewe  Katika safari yangu  Tatembea na wewe . Pamoja na Wewe  Pamoja na Wewe   Katika safari yangu Tatembea na Wewe. Mali hapa sikutaka  Ili niheshimiwe Na yanikute mashaka Sawasawa na Wewe  Pamoja na Wewe   Pamoja na Wewe   Heri nikute mashaka Sawasawa na Wewe. Niongoze safarini Mbele unichukue Mlangoni mwa mbinguni Niingie na Wewe   Pamoja na Wewe (2x) Mlangoni mwa mbinguni  Niingie na Wewe .